Hili ndilo kosa ambalo lilisababisa kukamatwa kwa Rose Muhando

Msanii maarufu wa nyimbo za injili Rose Muhando anazuiliwa na polisi mkoani Singida baada ya kukamatwa  kwa kupata pesa kwa njia ya udanganyifu.

Kwaya ya AICT Singida ilimshtaki Rose Muhando kwa kuwalaghai Tsh. 800,000. Muhando alilipwa laki 800 kwa njia ya M-Pesa kwa makubaliano angeweza kufika kwenye uzinduzi wa kwaya ambao ulipangwa kufanyika November 8 mwaka jana lakini hakufanya hivyo.

Rose Muhando

Kwaya hio ingefaa kuongezea Muhando laki 150 ingine baada kufika kwenye uzinduzi huo. Mwimbaji huyo hata hivyo hakuweza kufika kwenye uzinduzi huo na pia hakurejesha laki 800 alizolipwa.

Jeshi la Polisi mkoani Singida linamzuia Rose Muhando kwa kituo cha polisi kwa mahojiano kufuatia tuhuma zinazomkabili.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.