Dully Sykes aeleza kwanini anaegemea upande wa Diamond badala ya Ali Kiba

Dully Sykes ameshawahi kushirikiana na Ali Kiba na Diamond kuachia nyimbo; ‘Kuteseka Nimechoka’ (na Ali Kiba) na ‘Utamu’ (na Dianond na Ommy Dimpoz).

Sykes pia amejaribu mara nyingi kuwapatanisha Diamond na Ali Kiba lakini kila mara alipojaribu juhudi zake ziliambulia patupu.

Dully Sykes na Diamond

Akiongea kwenye kipindi cha 180 Power cha Sibuka FM, Dully Sykes alifunguka na kusema kuwa anaegemea upande ya Diamond kuliko upande wa Ali Kiba.

Mwimbaji huyo alieleza kuwa upande wa Ali Kiba hawataki kuwa karibu lakini upande wa Diamond wanamuonyesha upendo

“Upande wa Alikiba hawataki kuwa karibu na mimi ila upande wa Diamond wapo karibu na mimi, sababu hao wapo karibu na mimi na wao wananionyesha upendo ndio maana nipo karibu nao na sina tatizo na Ali Kiba wala Diamond,” alisema Dully Sykes.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.