Nyota Za Warembo Hawa Zazidi Kung’aa Zaidi (picha)

Katika kuonyesha kuwa kweli wanajitihada ya kazi wanazofanya warembo Elizabeth Michael ‘Lulu’,Vanessa Mdee ‘Vee Money’ na Jokate Mwegelo wamekuwa mfano wa kuigwa na jamii kwa ujumla kutokana na jitihada zao na uwezo wao wa kufanya kazi na zikaonekana na jamii.

Haya ni baadhi ya mafanikio waliyofikia warembo hawa ambao wanahitaji pongezi:

  1. Vanessa Mdee
Vanessa kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram leo hii ametangaza kuwa ataungana na hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam ambapo atakuwa Balozi wa Hoteli hiyo, hayo ni mafanikio mazuri sana kwa Vanessa na anastahili pongezi. 

2. Jokate Mwegelo

Jokate Mwegelo amechaguliwa kuwania Tuzo za Vjana 100 wenye ushawishi mkubwa Africa(100 Most Influential Young Africans) kama Mfanyabiashara kupitia kampuni yake ya Kidoti. Hivi sasa Jokate yupo nchini Marekani kwaajili ya kushiriki Mkutano unaojulikana kama Forbes Under  30 Summit kwaajili ya kukutana na Vijana Wafanyabiashara kutoka nchi mbalimbali.

3. Elizabeth Michael

Elizabeth Michael kupitia Azam TV amechaguliwa kuwa Balozi wa Tamasha la tuzo za filamu kwa upande wa Africa Mashariki ikimaanisha kuwakilisha Tasnia ya Filamu za Bongo Movie katika Tuzo hizo.

Wanawake wote hawa warembo wamethubutu na wameweza na ni vyema kuwapongeza mara kwa mara katika Jamii Zetu.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.