Huddah Aweka Wazi Hisia Zake Kwa Juma Jux

Mfanyabiashara na mrembo kutoka Kenya Huddah Monroe amefunguka na kuelezea wazi hisia zake juu ya mwanamuziki kutoka Tanzania Juma Jux.

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na kituo cha televisheni cha East Africa, Huddah amefunguka na kueleza kuwa Jux ni mwanaume anayeweza kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi.

Ninavutiwa sana na style ya mavazi ya Juma Jux, yaani walahi his style is on point yaani mimi binafsi sijawahi kumtumia mwanaume meseji lakini siku moja naangalia picha kwa Instagram nikamtumia meseji nikamwambia unapendeza, yaani kila anachovaa kinampendeza. Mimi napenda mtu awe  na style yake mwenyewe yaani havai kama watu wengine wanavyovaa na akijitahidi hiyo style yake itakuja kumpeleka mbali sana”.

Pia kwenye mahojiano hayo, Huddah aliulizwa kama Jux ni aina ya mwanaume ambaye anaweza akawa na uhusiano naye wa kimapenzi alikiri kuwa anavutiwa naye kimapenzi pia kwa sasa yupo single akimaanisha hana mpenzi yoyote.

Ingawa hiyo inaweza ikawa ngumu kidogo kwa upande wa Jux kwani tetesi zinazoendelea kuenea hivi sasa ni kuwa amerudiana na ex wake Vanessa Mdee ingawa Vanessa amekataa lakini za chini ya kapeti zanadai kuwa Jux na Vanessa waliopo kwenye tour ya Fiesta pamoja inasemekana wana ukaribu uliopitiliza urafiki wanaodai wanao, kwani pia wawili hao walishasema kila mmoja kwa wakati wake bado anampenda mwenzake lakini huwezi jua tusubiri tuone.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.