Diamond Aelezea Kiundani Kuhusu Kolabo Yake na Rick Ross

Mwanamuziki anayezidi kufanya vizuri na kung’aa zaidi kwenye mziki wa bongo fleva, Diamond Platnumz kwa mara ya kwanza amefunguka zaidi kuhusiana na kolabo yake na Rick Ross.

Hivi karibuni Diamond alionekana kwenye video mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii akifanya video na rapa maarufu kutoka Marekani Rick Ross. Diamond aliyesafiri kwenda Marekani wiki mbili zilizopita alionekana akirekodi video na Rick Ross lakini hakutoa maelezo yoyote.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Dizzim Online Diamond alifunguka yafuatayo;

Joseph Kusaga ndiye aliyenitafuta na kuniambia kuwa Rick Ross anataka kufanya kolabo na mimi lakini kwa kipindi kile nilikuwa kwenye process ya kutengeneza ngoma yangu hii mpya ya Hallelujah ambapo nilikuwa nimeshatengeneza verse moja na chorus basi nikaelekea nchini Rwanda kwaajili ya Fiesta, pamoja na kwamba ngoma yangu ya hallelujah nashukuru ilipokelewa vizuri niwashukuru mashabiki zangu lakini bado nilikuwa na njaa zaidi so nikapanda ndege mpaka Marekani ambapo nilikutana na Rick Ross na nimemshirikisha kwenue nyimbo yangu mpya itakayotoka hivi karibuni lakini sitaki kusema vitu vingi sana kwa sasa nataka iwe surprise kwa mashabiki zangu lakini wategemee mambo mazuri”.

Diamond pia ameongelea shoo zake anazotegemea kufanya mwaka huu kwenye  nchi mbalimbali kama Dubai, Marekani.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.