Waziri Mwakyembe- Diamond Anaanza Kulewa na Umaarufu

Waziri wa Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo, Mh. Harrison Mwakyembe, amemuoa juu staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz kutokana na kauli zake alizozitoa kwa Naibu Waziri Juliana Shonza.

Dkt. Harrison Mwakyembe ameelezwa kukerwa na kauli alizozitoa Diamond ambazo anaamini zinamdhalilisha Naibu Waziri Juliana Shonza wakati akihojiwa na kipindi cha The Playlist cha Times Fm.

Dkt. Mwakyembe amefunguka na kudai anaona staa huyo wa Bongo fleva ameanza kulewa umaarufu hadi kufikia hatua ya kumdhalilisha kiongozi wa serikali:

Dkt. Mwakyembe ameongea haya na Global Publishers:

Kama ni vikao na wasanii tumefanya vingi sana, lakini Diamond haudhurii vikao hivyo sio wajibu wa serikali kumfanyia kikao chake mwenyewe, however popular he is hatuwezi kuwa na sheria kwa wasanii wengine na sheria maalumu kwake, nadhani hizi ni dalili za kuanza kulewa umaarufu kwani Diamond sio kiongozi wa shirikisho la muziki wala msemaji wa Chama cha muziki wa kizazi kipya kuwasemea Wenzake. Si busara kwake kushindana na serikali na kama ana ushauri basi atoe kistaarabu utazingatiwa lakini si kwa kumshambulia Naibu Waziri kwa dharau na kejeli jinsi alivyofanya sijafurahishwa hata kidogo”.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.