Dj Rasta Bob Wa Uganda Adai Zari Alikuwa Mpenzi Wake Kabla Hajamuacha na Kukimbilia Wanaume Matajiri

Dj na mtangazaji maarufu nchini Uganda Robert Ogwel maarufu kama Dj Rasta Bob Mc amefunguka na kudai Ex wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zari alikuwa mpenzi wake kabla hajamuacha na kwenda kwa Ivan.

Dj Rasta Bob alimwaga ubuyu huo Kwenye mahojiano aliyofanya hivi karibuni na kituo cha Spark Tv nchini Uganda ambapo alidai yeye ndio alikuwa mwanaume wa kwanza kuwa na Zari.

Dj huyo amefunguka na kudai kuwa yeye ndio alimtoa Zari kwao Jinja na kumleta jijini Kampala nchini Uganda kutokana na kuvutiwa na urembo wake lakini pia amedai kuwa yeye ndio alimfunza mambo mengi Zari kuhusu ustaa kwani kipindi hiko alikuwa maarufu sana.

Lakini pia amedai muda mfupi baada ya kuwa wa mjini na kupendeza ndipo Zari alivyomtosa na kuanza kutoka kimapenzi na mwanaume tajiri ambaye ni Ivan na kumwambia anaweza kuishi mwenyewe mjini na kumuacha solemba.

Dj Rasta ambaye ni mkongwe nchini Uganda katika sekta ya burudani amekiri pamoja kuwa Zari amefanikiwa kimaisha na kutoka na wanaume matajiri lakini watambue kuwa yeye ndio alimtoa kijijini na kumfundisha kila kitu kuhusu kuishi mjini.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.