Zari Awaonya Wasafi Tv Kuwa “ Endapo Mtaendekeza Kiki za Kijinga Mtapotea”.

Mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz Zarinah Hassan ‘Zari’ amekitolea uvivu kituo cha Wasafi Tv.

Bila kujaribu kuwa mmiliki wa kituo hicho cha habari ni Diamond, Zari amewajia juu akiwataka kuripoti Habari za maana kuhusu mambo yanayoendelea nchini.

Zari alitoa povu hilo baada ya Wasafi Tv kuposti clip ya kipindi cha Refresh kinachorushwa na kituo hiko kikionyesha mahojiano waliyofanya na video Queen maarufu Irene Au Lynn.

Kwenye mahojiano hayo Irene aliulizwa endapo anamfahamu Zari ambapo alijibu kuwa hamjui Zari wa hajawahi kumsikia ambapo alisikika akisema ‘Zari Who?’.

Baada ya clip hiyo kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii Zari alienda kwenye ukurasa wa kituo hicho na kuwataka waripoti mambo ya maaan yanayoendelea Kwenye jamii badala ya kukazania mambo ya kijinga.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.