Mbosso- Nyimbo Zangu Hazipigwi Redioni

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Maromboso au maarufu kama Mbosso ameongelea Kitendo Cha nyimbo zake kutopigwa na baadhi ya media.

Mkurugenzi wa WCB Diamond Platnumz amekuwa kwenye mgogoro na baadhi ya vyombo vya habari hadi kupelekea nyimbo zake kufungiwa na vituo hivyo.

Wasanii wote ambao wako chini ya WCB wamekuwa wakibaniwa nyimbo zao kupigwa Kwenye Media hizo na Mbosso akiwa mmoja kati ya wasanii hao.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Mbosso ameweka wazi kuwa ingawa  nyimbo zake hazipigwi na baadhi ya media lakini anashukuru zinadai kila vyema kwa mashabiki zake.

Ukizungumzia moja ya wasanii ambao hawakupata bahati ya kupata nafasi kubwa kwenye radio station, mimi pia naweza kusema nipo.

Sikupata bahati kabisa nyimbo kupigwa kwenye radio station lakini wananchi wamenipokea, wamesema Mbosso tunakusapoti, wamenisapoti nashuru leo nimefika nilipofika”.

Baada ya media zaidi ya nne kugoma kupiga nyimbo za Diamond na wasanii wote wa WCB, Diamond alifikia uwaumuzi wa kufungua Stesheni yao ya Wasafi Tv.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.