Banana Zorro Afunguka Baada Ya Kuonekana Amevaa Msalaba

Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Banana Zahir Zorrro amefunguka baada ya kuonekana akiwa amevaa msalaba wenye picha ya Yesu Kwenye shoo.

Banana Zorro amezua gumzo usiku mnene ukumbini baada ya kuonekana akiwa ametinga msalaba shingoni wenye sanamu ya Yesu Kristo msalabani huku ikifahamika kuwa ni Muislam.

Jambo hiko liliibua maswali kwa mashabiki zake ambao walitinga Kwenye shoo yake iliyofanyika Ukumbi wa Legend Park, Namanga jijini Dar es Salaam.

Kwenye mahojiano na Global Publishers Banana Zorro alifunguka na kuweka wazi kuwa yeye ni muislamu lakini aliamua kuvaaa rozari ile kwa sababu alizawadiwa na Marehemu mama yake:

Ni kweli mimi ni Muislamu  lakini huu msalaba ukweli ni wa Kikristo aliniachia marehemu mama yangu mzazi kwa kuwa alikuwa Mkristo“.

Banana ambaye ametokea kwenye familia ya wanamuziki kuanzia baba yake mpaka dada yake Maunda Zorro.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.