Bifu Laibuka Baada Ya Kundi La Makomando Kuvunjika

Kundi la muziki la Makomando lililokuwa maarufu kwa uchezaji wa staili yao ya Kibega lililokuwa linaundwa na wasanii kama vile Muki, Fred, Msami Baby na wengineo limevunjika rasmi.

Makomando walitangaza kundi hilo kuvunjika mwaka jana mwishoni na tangia hapo bifu zito na ushindani umeibuka baina ya wasanii waliokuwa wanaunda kundi hilo.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Msanii aliyekuwa anaunda kundi hilo Fred amefunguka kueleza sababu ya kundi hilo kuvunjika na kupelekea kila mmoja kuwa adui wa mwenzake.

Kundi la Makomando limevunjika tangu mwezi wa 12 mwaka jana kila mtu amechukua hamsini zake anafanya kazi zake binafsi.

Lakini pia Fred amefunguka na kuelezea bifu lake na Muki linaloendeela ambapo siku za nyuma aliwahi kumdiss sana Kwenye vyombo vya habari kuhusu kazi zake na kudai hawezi kurudi tena Kwenye chati maana alikuwa anategemea kundi.

Fred ameongelea ushindani na bifu linaloendelea kati Muki na Msami na kuweka wazi kuwa hamna ushindani kati ya Muki na Msami Baby kwani ni wazi kuwa Msami ni mkali kuliko Muki.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.