“Ali Kiba ni Msanii Mkubwa na Amenifundisha Mambo Mengi Kwenye Muziki”-Barakah The Prince

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amempa heshima msanii mkongwe wa Bongo fleva Ali Kiba na kudai ni msanii mwenye experience kubwa Kwenye Bongo fleva.

Barakah alikuwa chini ya Label ya Rockstar 4000 ambayo inaendeshwa na Ali Kiba lakini baada ya miaka michache ndani ya Label hiyo BAraka alitangaza kujitoa na kuanza kufanya Muziki wake mwenyewe.

Baada ya kutoka Rockstar Baraka aliwatuhumu kwa kufanya njema mbali mbali za kumrudisha nyuma kimuziki ikiwemo mapema mwaka huu aliwatuhumu kwa kufuta nyimbo zake Youtube.

Lakini sasa inaelekea Baraka amerudi katika nafasi nzuri na Ali Kiba kwani Kwenye Interview yake na kipindi cha refresh cha Wasafi Tv, Baraka amemtaja Ali Kiba kama mtu aliyemfundisha mambo mengi kwenye sanaa kutokana na experience yake;

Ali Kiba ni mkubwa na ana experience Kwenye Industry more than me kwaiyo muda ambao nilikuwa naye nilijifunza vitu vingi Kimuziki na kusema kweli nilikuwa niijua thamani yangu kama msanii na nilijua nini natakiwa kufanya ili kufanikiwa maana yeye ameshakula matunda ya Muziki wetu”.

Barakah amesema kwa sasa hana mpango wa kusainiwa chini ya label yoyote hapa Tanzania labda hapo baadae.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.