Esma Platnumz Amkingia Kifua Wema

Dada wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Platnumz ameibuka na kumkingia kifua Wema Sepetu kutokana na sakata linaloendelea hivi sasa Kwenye mitandao ya kijamii.

Siku ya juzi Wema alimtambulisha mpenzi wake mpya ambaye amedai ndiye atakuwa mume wake mtarajiwa lakini moja kwa moja hali ilibadilika kwani mwanaume yule ameshawahi kumtukana Wema.

Mashabiki mbali mbali wa Wema walimshauri avunje Mahusiano na mwanaume yule na wapo hata Mastaa Wenzake ambao walimshauri atulie kwani mwanaume yule tayari ana wake wawili.

Lakini Esma ameibuka na kumpa sapoti Wema na kulpongeza kwa maamuzi  yake na kumtaka kufanya  kile ambacho moyo wake umeridhia na kama anataka Kuolewa na yule mwanaume basi ruksa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Esma ameandika maneno haya kwenda kwa Wema:

Go go Mu forever wiii cha muhimu ukiwa naye uko happy, ifike mahali tuheshimu hisia za watu jamani tutapangiana maisha mpaka lini? Insta imekuwa sehemu ya watu kutuchagulia maisha watu tuishi vipi khaaa Wema ngoja na mimi nikitoe kibabu changu”.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.