“Chiddi Ameletwa na Mungu ‘Special’ Kwaajili Yangu”- Shamsa Ford

Msanii wa filamu za Bongo movie mwanadada shamsa Ford ameibuka na kudai anampenda sana mumewe huyo na anaamini ameletwa maalumu kwa ajili yake.

Lakini pia Shamsa amedai kuwa anaamini kama bila kumuweka ndani huenda hadi leo angekuwa amedoda kwa kitoolewa kwani kwenye ulimwengu huu haoni kama kuna mwanaume aliyestahili kuwa mumewe.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Shamsa alisema kuna sababu nyingi za kumfanya aseme hivyo kubwa ikiwa ni jinsi mwanaume huyo anavyompenda kwa dhati kiasi kwamba anaamini ame­letwa na Mungu spesho kwa ajili yake.

Hata kama dunia ingeisha leo na tukarudi mara ya pili mimi bado nin­gemchagua mume wangu Chid kwa sababu naona ndiye mwanaume pekee aliyekuja kwa ajili yangu. Ananipa furaha isiyo kifani kiasi kwamba naamini kama asingetokea yeye, mpaka leo ningekuwa sijaolewa, yaani ningekuwa bado nas­ubiri aje hata angechelewa vipi”.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.