Monalisa na Mwanaye Washangaza Umati Kwa Hili

Msanii mkongwe wa Bongo movie Yvonne Cherry maarufu kama Monalisa na Mtoto Wake Sonia walishangaza watu Baada ya kuonekana wakiangua kilio mbele ya hadhara.

Monalisa na Mwanaye walishikwa na huzuni na kuanza kulia walipokuwa wakikabidhi misaada kwenye kituo cha kulea watoto yatima cha Yoko kilichopo Mbezi- Mwisho jijini Dar.

Aliyeanza kulia ni mtoto wa staa huyo, Sonia baada ya kupewa kipaza sauti azungumze ambapo alishindwa, akaanza kulia huku mama yake akimkumbatia, wakajikuta wakilia pamoja na baadae Watoto wa kituo kile nao walionekana wakilia.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, rafiki wa karibu wa Sonia ambaye alikuwa ameongozana nao alitoa sababu iliyomfanya mpaka akaanza kulia:

Masikini Sonia, anaonekana ana huru­ma na machozi yanamtoka kwa sababu na yeye anakumbuka amempoteza baba yake pia”.

Monalisa alifunguka na kusema kuwa ameamua kujitoa kusaidia wazo hilo la mtoto wake kwa sababu ameona anafanya jambo jema.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.