Ali Kiba Awataka Radhi Mashabiki Wake

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri hivi sasa Ali Kiba amefunguka na kiwataka radhi mashabiki zake wote.

Ali Kiba aliomba radhi baada ya kushindwa kutimiza ahadi yake ya kufanya tamasha la Funga mwaka na King Kiba baada ya kudai kupatwa na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wake na hivyo kupalelekea kukosa kishiriki tamasha hilo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ali Kiba aliandika ujumbe huo wa msamaha na kuonyesha kusikitishwa na kitendo cha kishindwa kushiriki tamasha hilo:

Hello fans  natumaini kila mmoja wenu amekuwa na wakati mzuri katika kipindi hiki cha sikuku ningependa kuchukua nafasi hii kiwaomba radhi kwa kishindwa kuwatimizia kifanya Funga mwaka na King Koba kama ilovyohaidiwa. Haikuwa lengo langu ila kuna mambo yamejitokeza  yaliyo nje ya uwezo wangu ambayo yamesababisha kitoweza kufanyika kwa tukio letu ambalo lingehusisha uzinduzi wa bidhaa zangu na wimbo wangu mpya. Hata hivi karibuni Mungu akijaalia ntawapa taarifa ya namna tutakavyoufungua mwaka  asanteni sana kwa ushirikiano na support mnayonipa kila siku Mungu awabariki sana”.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.