Alichosema staa wa filamu Bongo,Lulu kuhusu ‘kuachana’ na mchumba wake

Stori za mitaani kuhusu uchumba wa Elizabeth Michael,ajulikanaye kwa jina Lulu,mkali wa filamu Tanzania,kukatika zimemkwaza na kumpandisha hasira sio mchezo.

Inaripotiwa kua sio mapenzi mubashara tena kati yake na mpenzi wake,baada ya wawili hao kutemana kama big G.

Elizabeth Michael na Majizo

Kwa mujibu wa taarifa hii,mambo sio kama kawaida kwani pendo limevunjika huku kila moja akiongea lake.

Madai kuwa staa huyo wa filamu na mpenzi wake kuonyeshana kisogo yalienea kwenye mitandao ya kijamii huku wadaku wa town wakiongeza makali na pilipili zaidi na kudai kuwa, Lulu karejea nyumbani kwao na ana mpango wa kuanzisha maisha yake upya.

Staa huyo amekereka kuhusu stori hii,haya ndio maneno yake kwa wanahabari wanaotaka kujua kulikoni.

“Sitaki kuongelea chochote…sitaki kuongelea chochote, pliz…unajua mimi siyo mtu wa magazeti kabisa na unanijua vizuri…” amesema Lulu.

Kumbe hapendi stori za magazeti?

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.