Alichosema Young Killer baada ya Diamond kuamua kutoa wimbo naye

Nyota ya Young Killer sasa inakaribia kung’aa vizuri, rapa huyo ataingia studio na Diamond Platnumz kurecord ngoma mpya itakayompa umaarufu nje ya Tanzania.

Msanii yeyote ambaye amewahi kufanya kazi na Diamond anajua vizuri thamani ya kumshirisha Simba kwa kolabo yoyote ile.

Young Killer

Young Killer sasa amefunguka kuhusu kazi atakayofanya na hit maker huyo wa ‘Marry You’. Rapa huyo alisema mama yake alifurahishwa sana na kitecho cha Diamond kuamua kumshirikisha kwenye moja kati ya nyimbo zake zinazokuja.

Akiongea na Bongo5 hapo jana Mai tarehe nne, Young Killer alimmwagia sifa Diamond na kumtaja kama msanii anayekuza vipaji Tanzania.

“Hiki kitendo kimenifanya nimuone Diamond Platnumz ni binadamu na ni mtu ambaye anastahili kuwepo sehemu ambayo yupo. Ni tukio ambalo limenitia faraja kiukweli hata mama yangu alivyosikia alifurahia sana na kumshukuru kwa kitendo ambacho amenifanyia,” alisema Young Killer.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.