Baada Ya Kimya Kirefu Alikiba Adokeza Wimbo Mpya

Mwanamuziki wa Bongo fleva Ali Kiba amefunguka kuhusu kimya chake baada ya kutotoa nyimbo mpya tangu mwaka jana mwezi wa nane mpaka hivi sasa.

Wimbo wa mwisho Ali Kiba kutoa ulikuwa hit Single yake ‘Seduce me’ tangia hapo mashabiki zake wamekuwa na juu kubwa ya wimbo mpya.

Siku ya Jumapili tarehe 29/4 ilikuwa ni reception ya Harusi yake na hapo aliwang’ata sikio mashabiki zake kwa kukiri kuwa anajua mashabiki zake wana kiu ya nyimbo mpya lakini kuna. Vitu vingine amewaandalia.

Kitu ambacho naweza nikawaeleza tumefanya mambo mengi katika ukimya wangu, najua watu walikuwa wanasubiria wimbo mpya itoke lakini pamoja na hayo kuna vitu vipya nimejihusisha navyo katika biashara ambayo naifanya”.

Ali Kiba alizindua kinywaji chake kipya kinachoenda kwa Jina la Alikiba Mo Faya Energy drink Ikiwa ni moja ya hatua zake za kujiingiza Kwenye ulimwengu wa ujasiriamali.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.