Baada Ya Kushinda Tuzo Mbili Wema Sepetu Alamba Shavu Hili Tena

Muigizaji wa Bongo movie mrembo Wema Sepetu amelamba  shavu jingine siku ya jana baada ya kutangaza kuwa filamu yake ya Heaven sent itauzwa kwa mfano wa DVD ili kuwafikia watazamaji wengi.

Wema alijishindia tuzo mbili wikiend iliyopita kutoka katika tuzo za Sinema Zetu International Film Festival (SZIFF) ambazo ni Muigizaji bora wa kike 2018-2019 na People’s choice Award (Chaguo la watu).

Lakini inaonekana huo ulikuwa mwanzo tu wa baraka za Wema kwani jana kwenye mkutano na waandishi wa habari Wema ametangaza kupata dili jingine na Azam Tv likiwa ni Kusambaza movie yake kwenye mtindo wa DVD.

Tangu movie ya wema imetoka mapema mwaka jana amekuwa akiiuza filamu hiyo kwa mtindo wa digitali kumaanisha amekuwa akiuzia filamu hiyo Kupitia App yake ya Wema Sepetu inayopatikana kwa simu za Android.

Wema amehaidi kufanya filamu full time na kuhakikisha analeta mambo mazuri katika tasnia hii ya Bongo movie lakini pia Kumekuwa na tetesi kuwa mwezi wa Sita ana mpango wa kuzindua filamu yake aliyoigiza na Van Vicker.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.