Baada Ya Rommy Jones Kumtongoza Naj, Mkewe Kasema Hana Mpango Wa Kumuacha

Siku ya leo Romy Jones ambaye ni kaka wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz ameingia kwenye headlines baada ya meseji zake akimtongoza msanii wa Bongo fleva Naj kuvujishwa Instagram.

Kwenye meseji hizo Rommy anamtaka Naj ambaye ana  uhusiano wa kimapenzi na Msanii wa Bongo fleva Barakah The Prince ambapo amemponda na kudai Barakah anashusha nyota yake.

Rommy Jones alimuoa mkewe Miezi michache iliyopita ambaye anajilikana kama Kay Jord kwaiyo baada ya skendo yake ya kumtaka Naj ambaye pia ni Ex wa kaka yake Diamond kutokea iliwashangaza watu wengi.

Baada ya sakata hilo kutokea asubuhi hii Kay ametumia ukurasa wake wa Instagram kujulisha watu kuwa hana Mpango wa kuachana na mumewe ambapo ametumia msemo unaosema:

Kumuacha mwanaume kisa anaku cheat ni sawa sawa na kukimbia nchi kisa mvua inanyesha kwani mvua hunyesha kila sehemu”.

Akimaanisha wanaume wote wanachepuka hivyo hawezi kumuacha mumewe kisa na mjadala kachepuka.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.