Baba Diamond Atoa Neno Kuhusu Ndoa Ya Diamond na Tanasha

Baba mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Mzee Abdul Juma maarufu kama Baba Diamond amefungukia Ndoa Ijayo kati ya Mwanaye Diamond na Mpenzi Wake Tanasha Donna.

Wiki chache zilizopita Diamond alitangaza rasmi kwenye mitandao ya kijamii dhamira yake ya kumuoa mrembo kutoka nchini Kenya, Tanasha Donna ‘Zahara Zaire’ ifikapo Februari mwakani na kufanya watu wengi kuwa na hamu ya kushuhudia harusi hiyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi, Baba Diamond amesema ingawa Mpaka sasa hajapewa taarifa kuhusu Ndoa ya mwanaye lakini anatamani siku ya Ndoa wamualike.

Sijaambiwa habari za ndoa ila nasikia tu watu mitaani wanazungumzia suala hilo, kikubwa naomba iwe ya heri Mungu afanikishe nitafurahi sana mwanangu akioa lakini namuomba sana asiache kunialika, asiponialika nitaona amenidharau sana, nitajisikia vibaya”.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.