Babu Tale Atiwa Mbaroni.
Meneja wa kampuni ya Tip Top Tanzania Babu Tale almaarufu amejikuta akiingia matatani baada ya kuwa anasakwa kwa muda mrefu huku sababu kubbwa ikiwa ni kesi inayohusiana na kesi ya madai.Babu tale na mdogo wake Idd Taletale waliamuliwa kukamatwa na mahakama tangu tarehe February 16 mwaka huu na naibu katibu msajili wa mahakama kuu baada ya kupokea kesi ya madai kutoka kwa Sheikh Hashim Mbonde.
Hata hivyo tangu kulipotolewa mari hiyo ya mahakama Babu Tale na ndugu yake wamekuwa wakitafutwa na bila mafanikio ya kupatikana mpka walikamatwa siku ya May 21 mwaka huu na kupelekwa mahabusu moja kwa moja huku wakisubiri kuitwa tena mahakamani.
Mahamani kuu ambayo ilimuamuru babu tale kumlipa Sheikh Hashim Mbonde faini ya shilingi milion 250 za kitanzania kutokana na kesi ya madai baada ya kukutwa na hatia ya kutokuwa na hakimili ya kutumia masomo ya mhadhili huyo wa dini katika shughuli zao za kibiashara bila kuwa na ruhusa yake mwenyewe.
May 22 Babu Tale alifikishwa mahakamani ili kusikilizwa kwa kesi hiyo iendelee na kusikiliza hukumu lakini kesi hiyo ilihairishwa na Babu Tale kurudishwa mahabusu kwa sababu naibu msajili aliyetoa amri ya kukamatwa kwake kutokuwepo mahakamani hapo.