Beka Flavour: Aslay si msanii mkubwa kwamba mimi nimuogope. Ali Kiba ndo anaweza

Msanii Beka Flavour sasa anavurugana na Aslay kuonyesha ubabe katika muziki. Bifu yao ni kama ile ya Ali Kiba na Diamond igawa bado haiwezi.

Ubishi kati ya Beka Flavour na Aslay unadhihirika jinsi wanavyoachia nyimbo zao zikifwatana. Akiongea na eNewz, Beka Flavour alisema hawezi kumruhusu Aslay kutoa ngoma bila yeye kuachiza nyimbo zake zishindane na za hasimu wake.

“Nimepanga kuachia wimbo mpya wiki mbili zijazo lakini kama Aslay akiachia tena kazi mpya sitaweza kumvumilia na mimi nitaachia mashine ili zipambane mbele kwa mbele maana mimi nimeshapanga ratiba zangu na siwezi kuzivunja,” Beka Flavour alisema.

Beka Flavour

Staa huyo hata hivyo alisema Aslay sio msanii mkubwa wa kumuangalia wakati anafanya kazi zake, alidai kuwa Ali Kiba ndiye kioo chake Tanzania.

“Mimi natoa nyimbo zangu kulingana na jinsi ambavyo nimepanga ratiba yangu na uongozi wangu. Sijashindwa kuachia wimbo eti kwa sababu Aslay katoa ngoma mpya ila matatizo niliyopata ya kupelekwa polisi ndiyo yaliyonifanya nisogeze vitu mbele. Aslay siyo msanii mkubwa kusema kwamba mimi nimuogope au nimfikirie. Hapa nchini msanii mkubwa ni Alikiba na ndo kama kioo najitazama lakini siyo Aslay. Mimi natazama wasanii wakubwa nje ya nchi lakini siyo ndugu yangu,” Beka Flavour alifunguka.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.