Ben Pol Amenifundisha Muziki:-Paul Clement

Msanii wa muziki wa injili Paul Clement amefunguka na kusema kuwa hakuwahi kujua kama angeweza kufanya vizuri katika muziki ila kwa msaada wa msani wa bongo  fleva Ben Pol aliweza kufanikiwa katika muziki kwa sababu aliweza kumsaidia na kumfunidsha kuimba.

Paul Clement hakuona aibu alipokuwa akiongea na kipindi cha Pambio Live cha Kenya kuhusu kukua kwake kimuziki tangu anaanza kufanya muziki.

Ben Pol alinifundisha muziki,yeye ndio alinifundisha kuimba.Nilikuwa nikienda katika mashindano fulani kuimba nikawa nafukuzwa stageni na ninaambiwa kabisa toka haujui kuimba nenda kajifunze kuimba.Lakini Ben Pol alinifundisha kuimba na nilirudi palepale waliponiambia sijui kuimba nikaenda kuwaonyesha kwa sasa najua kuimba , nilitaka kuwaonyesha kuwa najua.Baada ya hapo nikaanza kuimba katika kundi moja la muziki wa injili la Glorious Celebration.

Sio kila msanii anaweza kuweka wazi kuhusu swala la yeye kufundishwa katika muziki tena hasa pale unapoiona kuwa status yako ni kubwa kwa mashabiki, wasaniiwengi wamekuwa waoga kukiri kuwa pale walipo kuna watu waliwahi kuwashika mkono nyuma yao.

Paul clement ni moja ya wasanii wakubwa wa injili wanaoimba kwa kutoa ujumbekatika jamii yake lakini pia amefanya muziki wake kuweza kupendwa  hata na nchi za jirani.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.