Billnas Afungukia Mahusiano Yake na Ali Kiba

Mwanamuziki wa Bongo fleva Billnas amefunguka na kuweka wazi kabisa uhusiano wake na staa wa Bongo fleva Ali Kiba.

Billnas amerudi Kwenye headlines huku safari hii Ikiwa ni uhusiano wake wa kikazi na Ali Kiba. Siku chache zilizopita kuna taarifa za sintofahamu zilisambaa kumuhusu Billnas na Ali Kiba.

Kwenye mahojiano na Kipindi cha Kikaangoni cha East Africa Tv, Billnas amefunguka kuhusu tetesi zilizodai kuna ngoma kati yake na Alikiba inakuja.

Nina Mahusiano mazuri na Ali Kiba na huwa ananishauri mambo mengi katika kazi zangu na hata muda mwingine huwa tunataniana naamini anakubali kazi zangu maana huwa nikiachia ngoma ananiambia mdogo wangu hapo freshi au kazia buti sehemu fulani.

Sitaki kuliweka sana hilo mbele ila watu wajue tunayo mahusiano mazuri kama nilivyo na mahusiano mazuri na wasanii wengine“.

Billnas anayefanya Muziki wake katika miondoko ya kurap anafanya vizuri hivi sasa na ngoma yake ya ‘Tagi Ubavu”.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.