Bodi Ya Filamu Yamfungulia Wema Sepetu

Bodi ya filamu Tanzania siku ya leo imetangaza kumfungulia Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu Baada ya kumkingia kwa miezi kadhaa na kujihusisha na Shughuli zozote za kisanaa.

Akitoa uamuzi huo mbele ya vyombo vya habari, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania (TFB),  Joyce Fissoo, amesema  Wema amefuata maelekezo aliyopewa na bodi hiyo kwa asilimia 75.

Hatujamfungulia sababu ya huruma, tumemfungulia sababu amefanya tuliyoagiza kwa zaidi ya asilimia 75“.

Mwaka jana mwezi wa kumi Bodi ya filamu ilitangaza kumfungia Wema na kujihusisha na Shughuli zozote za kisanaa Baada ya Msanii huyo kusambaza picha zake za utupu katika Mitandao ya kijamii.

Kabla ya kufungiwa, Wema aliomba msamaha kutokana na tukio hilo ambalo lilitokea siku kadhaa nyuma ambalo lilimuonyesha akiwa faragha na mwanamme anayesemekana ni raia wa Burundi, aliyedai kuwa ni mume wake mtarajiwa.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.