Diamond Ampangishia Hawa Hoteli Baada Ya Matibabu

Msanii aliyewahi kutamba kwenye kibao cha ‘Ntarejea’ Hawa Said amedaiwa kukaa kwenye hoteli aliyopangishiwa na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Wiki chache zilizopita Diamond alitoa  zaidi ya milioni 400 kwa ajili ya matibabu ya mrembo Hawa ambaye alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya ugonjwa wa moyo.

Baada ya kumaliza matibabu na Kurudi nchini Tanzania, Hawa amepangishiwa hoteli ambapo atakaa kwa muda wa miezi mutate ili kuepusha usumbufu.  

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Jumamosi, mama wa Hawa, Ndagina Kapera alithibitisha mtoto wake kurejea salama kutoka nchini India alikokuwa kimatibabu akiwa na afya ambapo baada ya kutua amepangishiwa chumba hotelini kwa ajili ya kuepusha usumbufu wa kelele.

Hawa amepewa masharti ya kukaa sehemu iliyotulia, isiyo na kelele kutokana na tatizo lake la moyo hivyo amepangishiwa hoteli moja hapa jijini Dar (jina linahifadhiwa) na meneja wa Wasafi (Hamis Taletale ‘Babu Tale’) kwa muda wa miezi mitatu mpaka afya yake itakapotengamaa“.

Mama huyo ameweka wazi shukrani zake za dhati kwa Msanii Diamond Platnumz kwa Kuokoa maisha ya Mtoto Wake.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.