Dogo Janja: Davido ako na pesa lakini hajui kuvaa

Rapper Dogo Janja amemshambulia Davido kwa kile alichodai kuwa msanii huyo kutoka Nigeria hajui kuvaa licha ya kuwa na utajiri mkubwa.

Dogo Janja ni miongoni mwa wasanii wanaong’ara sana nchini Tanzania, hivi karibuni alipigiwa upata kuwa anang’ara sana kushinda Diamond Platnumz.

Davido

Soma pia: Picha 10 za Dogo Janja ambazo ni dhibitisho kuwa anang’ara kimavazi kushinda Diamond Platnumz

Akiongea akiwa Sibuka FM, Dogo Janja alisema Davido ako na pesa nyingi lakini hajui kupendeza kimavazi, alieleza kuwa mara nyingi nguo anazovaa Davido ni kama huwa zimetundikwa tu mwilini mwake.

Janja pia alisisitiza kuwa yeye ndiye anayeng’ara zaidi kushinda wasanii wote nchini Tanzania. Aliwataja G Nako, Jux kwa mbali na Joh Makini kama wapinzani wake kwa uvaaji.

Dogo Janja

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.