Esha Buheti Amlipua Jokate na Kudai Anaona Wivu Baada Ya Alikiba Kuoa

Muigizaji wa Bongo movie Esha Buheti ameibuka na kumtupia tuhuma nzito mrembo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ baada ya kudai kuwa tangu amehudhuria harusi ya staa wa Bongo fleva Ali Kiba na Amina mrembo huyo amekata naye mawasiliano.

Esha ni mtu ambaye ana ukaribu sana na familia ya Ali Kiba na hata kwenye harusi ya Ali Kiba alionekana mwanzo mwisho akishitiki kwani alienda hadi Mombasa.

Hapo nyuma kuna taarifa ilisambaa kuwa Esha ndiye aliyemtafutia mchumba huyo Ali Kiba (Amina) ingawa mwenyewe alishakataa na hata Ali Kiba na Amina waliweka wazi walikutana wenyewe Kwenye ndege.

Kwenye mahojiano na Shilawadu  Esha anadai kuwa tangu ahudhurie ndoa ya Ali Kiba basi Jokate kama kama kamkasirikia kwani zamani alikuwa anaangalia status zake WhatsApp lakini saivi ameacha.

Mimi na Jokate tukiongelea kuhusu kukutana basi tulikutana kama mara tatu tu lakini kama yeye ananichukia ni yeye tu lakini mimi siwezi kumchukia kwa sababu sio mimi niliyeoa aliyeoa ni Ali kiba, ingawa kabla alikuwa ana view status zangu lakini tangu niende Mombasa sijaona aki view tena Lakini sikuhangaika kuangalia kama ameniblock au vipi”.

Jokate hajaonekana aliposti kitu chochote Kwenye mitandao ya kijamii tangu harusi ya Ali Kiba hivyo pia hajajibu tuhuma hizi.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.