Esma Ashabikia Ndoa Ya Diamond na Tanasha

Dada wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Platnumz ameibuka  na kuweka wazi mapenzi yake kwa wifi yake mpya Tanasha na kuweka wazi kuwa kama kaka’ke huyo atachukua uamuzi wa kumuoa kwake yeye anabariki kwa sababu ni chaguo lake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Esma hadhani kama ni vyema kumchagulia kaka yake huyo mke, bali macho yake ndiyo yanaona wapi ni bora aangukie hapo na atakapopachagua na kumuonesha atampokea tu.

Unajua hata leo Diamond  akimtambulisha rasmi Tanasha kuwa anataka kumuoa, mimi kama dada, nitaona ni jambo la heri kwenye familia yetu ambayo kila kukicha tunamuombea apate mke bora”.

Diamond alianzisha mapenzi na binti huyo wa Kikenya Wiki chache  zilizopita  Lakini wamekwisha tangaza ndoa yao ambayo itafanyika mwezi wa pili mwakani.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.