Familia Ya Agnes Masogange Yadai Haijapokea Michango Ya Marehemu

Familia ya marehemu Agnes Gerald ‘Masogange’ imelalamika kuwa haijapokea michango yoyote iliyokusanywa kipindi cha msiba wiki chache zilizopita.

Ndugu wa marehemu Agnes Masogange wakiwemo wifi zake ambao ndio wanaishi na mtoto mmoja wa Marehemu anayeitwa Sania wamesema hawajapata taarifa zozote juu ya fedha ambazo zilichangwa na Kamati ya wasanii kwa ajili ya malezi ya mtoto.

Kwenye mahojiano waliofanya na Planet Bongo ya East Africa Radio, mmoja wa ndugu hao aliyejitambulisha kwa jina la Sada, wamesema hawajapata taarifa zozote kutoka kwa kamati hiyo iliyoundwa na wasanii ambayo pia ilisimamia kwa kiasi kikubwa mazishi ya Agnes.

Toka tumekuja hatujapata taarifa yoyote bado hatujawasiiana nao mpaka dakika hii labda mpaka tuwatafute”.

Lakini pia familia hiyo imesema ina mpango wa kuendelea kumlea mtoto huyo kwani hata kipindi cha uhai wa mama yake  walikuwa wanamlea.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.