Florah Afunguka Baada Ya H.Baba Kukiri Kumiss Uwoya

Msanii wa filamu za Bongo movie, Florah Mvungj amefunguka Baada ya mume Wake ambaye ni Msanii wa Bongo fleva H. Baba kukiri kumiss Ex Wake Irene Uwoya.

Siku chache zilizopita H-Baba kupitia  ukurasa wake wa Instagram aliweka picha ya Irene Uwoya kisha kuandika kuwa amemmisi, jambo lililowashangaza wengi kwani siku za nyuma kidogo aliwahi kumponda na kusema haoni ndani kwa mke Wake Flora.

 

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Florah Mvungi amedai haoni tatizo kwa Mume Wake kumkumbuka Aliyekuwa Mpenzi Wake isitoshe amedai yeye hana wivu.

Watu wanakuza mambo sana, mbona ni hali ya kawaida sana, ni kumbukumbu tu ambazo mtu zinamrudia, anafanya anachojisikia, ameona ni vyema kushea kumbukumbu zake na watu kwenye mitandao, sijaona shida yoyote na wala sijahisi wivu“.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.