Harmonize Adai Kuwa Yeye na Diamond Wanamiliki Hisa Sawa Sawa

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Harmonize amefunguka na kuweka wazi yeye na Bosi wake  Diamond Platnumz wanamiliki hisa pasu kwa pasu kwenye kampuni ya Zoom Production.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha redio cha A FM cha jijini Dodoma, Harmonize ameanika ukweli ambapo amesema kuwa wote wawili wamegawana hisa sawa kwa sawa.

Wazo la kuanzisha Production company ni langu na nilipolipata nilienda Africa ya kusini na Marekani kununua kamera na baadae nikaja kusambaa Diamond, Bro! mimi naona tunapoteza hela nyingi sana kwenye video, mimi nimepata wazo la kuanzisha kampuni ya Video Productions wewe unaonaje?“

Harmonize amesema Diamond akakubali wazo hilo na kwa kuwa alikuwa ameshanunua kila kitu alivyorudi Bongo alimrudishia nusu ya manunuzi na kwa muda huo anasema kuwa alikuwa ameshmtafuta Director Kenny.

Zoom Production ni moja ya kampuni zinazofanya vyema kwenye ulimwengu wa Burudani na haimilikiwi na Diamond pekee ilivyoaminika hapo awali bali na Harmonize pia ana mkono mule.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.