Harmonize Afungukia Ujauzito Wa Sarah

Msabii wa muziki wa Bongo fleva Kutoka katika Label ya WCB, Harmonize amefunguka na kutoa majibu kuhusu utata wa ujauzito wa Mpenzi Wake Sarah.

Wiki chache zilizopita Sarah alitupia picha zilizomuonesha ni wa kujifungua muda wowote. Kabla ya kutupia picha hiyo kulikuwa na madai na minong’ono mingi kuwa mchumba huyo wa Harmonize alikuwa haonekani mara kwa mara kwenye mitandao ya kijamii kama ilivyokuwa huko nyuma kwa sababu eti alikuwa analea mimba hiyo hivyo hakutaka kujitokeza hadharani.

Lakini alipohudhuria Birthday party ya Msanii Wolper Wiki iliyopita na kuonekana akiwa hana ujauzito maneno Mengi yalizuka na kushangaza wengi walioamini mzungu huyo ni mjamzito.

Baada ya kuzidi kwa minong’ono Gazeti la Ijumaa, lilimfuata Mpenzi Wake Harmonize ili kupata ukweli wa mambo ambapo alifunguka:

Sidhani kama kila kitu ni vizuri kukiweka kwenye hadhara. Ni jambo kubwa hilo, lakini ni la kifamilia zaidi.

Kama anavyoonekana, hajajifungua na hana mimba kweli. Mara kadhaa Sarah amekuwa akidaiwa kuwa mjamzito, lakini hazina ukweli”.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.