Hawa Afunguka Baada Ya Diamond Kumpa Milioni 50 Za Matibabu

Msanii wa Bongo fleva Hawa Mayoka aliyewahi kutamba katika ngoma ya Diamond Platnumz ‘Ntarejea’ amefunguka na kumshukuru Msanii huyo kwa msaada wake wa matibabu.

Wiki chache zilizopita Habari zilisambaa kuwa Hawa anaumwa hoi kitandani na kuomba msaada wa matibabu ambapo tatizo ni  ini.

Diamond amethibitisha Kupitia mitandao ya kijamii kuwa yupo katika harakati za kumpeleka Hawa nchini India kwa ajili ya matibabu na kusema anatoa zaidi ya Milioni 50 kwa ajili ya matibabu yake kutoka katika mfuko wake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda,  Hawa amesema kitendo cha Diamond kujitolea kumsaidia matibabu ya kumpeleka nchini India kimemliza mno kwa sababu hakujua kama ipo siku angemkumbuka.

Nilivyosikia Diamond ameamua kunisaidia nilijisikia furaha mpaka machozi yakawa yananitoka maana sikuamini, Mungu atamlipa na namuombea azidi kuwa na moyo huohuo.

Nilishakata tamaa kabisa ya kupata matibabu kutokana na uwezo wa kifedha kuwa mdogo kwani madaktari wa hapa walisema natakiwa kutibiwa India, kwa sasa nimepata tumaini jipya baada ya Diamond kujitolea kunipeleka kwenye matibabu India“.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.