Jeshi la Magereza Lakanusha Taarifa Za Lulu Kuwa Huru

Jeshi la magereza limekanusha taarifa zilizosambaa siku ya Jana kwenye mitandao ya kijamii kuwa Muigizaji wa Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu amekuwa huru baada ya kumaliza kifungo chake.

Kupitia kwa Msemaji Mkuu wa Jeshi hilo, Amina Kavirondo, amesema kuwa muigizaji huyo bado ni mfungwa kwani kuna utaratibu uliowekwa ambao atapaswa kuufuata ili aweze kuachiwa huru na

Kwenye mahojiano na kituo cha televisheni cha EATV, Bi. Amina amefunguka na kusema:

Taratibu nafikiri zinaeleweka, (Lulu) anakuwa bado ni mfungwa, na anapokuwa na kifungo hicho cha nje kuna taratibu zake, akimaliza basi kuna taratibu kama mfungwa yeyote, hata kama ni maarufu. Kile ambacho Lulu atafanyiwa ndicho atakachofanyiwa mfungwa mwingine yeyote, ‘treatment’ yetu ni sawa na wafungwa wengine”.

Lakini pia Bi. Amina amesema kuwa Lulu mwenyewe anajua taratibu za kufuata ili aweze kuachiwa huru:

Mwenyewe anajua anatakiwa afanye nini, yule ni mfungwa kama wengine, hawezi kumaliza akaondokea kule kule”.

Taarufa za Lulu kumaliza kifungo zilikuja baada ya kudaiwa kumaliza rasmi kifungo chake cha nje siku ya jana.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.