Lulu Afunguka Mazito Kuhusu Majizzo

Muigizaji wa Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu amefunguka na kuongea mazito kuhusu mpenzi wake ambaye ni Mkurugenzi wa EFM, Majizzo.

Mwanzoni mwa wiki hii Majizzo alimvalisha pete ya uchumba mpenzi wake wa siku nyingi Lulu Ikiwa ni Miezi Michache tangu alipoachiwa huru kutoka kwenye  kifungo chake baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia Steven Kanumba.

Baada ya kuvalishwa pete Lulu alifunguka mazito juu ya mpenzi wake Ikiwa ni pamoja na kumshukuru kwa kuwa naye hata katika kipindi kigumu maishani mwake.

Lulu amesema kuwa mpenzi wake Msjizz amemvisha pete ya uchumba hivi karibuni  kama Baba kwake kwani ni mtu wa kuvaa uhusika tofauti tofauti hadi kumfanya ajisikie upendo wa Baba.

Huku machozi yakimtiririka Lulu alifunguka:

Tokea nimeanza kuwa naye nimefeel upendo wa Baba Kwenye Maisha Yangu kwa sababu kuna muda anatoa character ya upenzi na Nini anakuwa kama Baba na kipindi kifupi kilichopita tulipita katika wakati mgumu sana lakini Tunashukuru Mungu”.

Ingawa mwaka huu ulianza vibaya kwa Lulu lakini unaelekea kuisha vibaya kwani Lulu amebakisha mwezi mmoja ili kumaliza kifungo chake cha nje na baada ya hapo inasemekana atafunga ndoa na Majizzo na kuna tetesi za ndoa kuwa Dubai.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.