Mama Diamond Amwaga Povu Kulinganishwa na Mobetto

Mama mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi. Sandrah maarufu kama Mama Diamond amemwaga Povu zito baada ya mashabiki wa mtandaoni kumlinganisha na aliyekuwa mkwe Wake Hamisa Mobetto.

Sakata hilo lilitokea siku chache zilizopita baada ya Mama Dangote kuweka picha mtandaoni zilizomuonyesha akiwa amebebwa na Mume Wake Shamte ndipo mashabiki walimtuhumu kwa kumuiga Mobetto.

Siku za nyuma kidogo Mobetto aliweka picha zake na Mpenzi Wake Josh Adeyeye zilizomuonyesha wakiwa wamebebana kimahaba ndipo walipounganisha na zile za Mama Dangote na kumtuhumu kwa kuiga.

Katika mahojiano yake aliyofanya Global Publishers, Mama Diamond alimwaga Povu zito Baada ya kuulizwa kuhusu tuhuma hizo:

Unajua siwezi kujibu swali hilo la ajabu, kwani wewe ukibebwa unajisikiaje? Na hayo mambo ya Mobeto jijibu mwenyewe na uandike unachojisikia“.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.