Mama Kanumba :Kanumba angekuwepo Angemuoa Wema.

Mama wa moja ya wasanii  waliokuwa waigizaji nguli Tanzania , mama Steven Kanumba amefunguka na kukanusha tetesi za kuwa yeye pamoja na Wema amabe aliwahi kuwa katika mahusiano na marehemu mtoto wake kuwa wana ugomvi sio kweli kwa sababu kama yeye Wema ni binti aliyetokea kumpenda sana.

kwakweli wema mimi sina bifu nae na hakuna binti ninaye mpenda kama wema,na ninaomba anielewe hivyo, tukionana tusalimiane na tupendane na hizo habari za kutokunifungulia mlango ni uongo, aache kunifungulia kwani mimi namdai au yeye ananidai.

Mama kanumba pia akanusha tetesi za kwenye mitandao kuwa amekuwa akiombamsaada kwa wema na kwamba amekuwa akienda mpaka nyumbani kwake.

Na wala sijawahi kuomba ela ingawa kuna wengine wanasema kuwa nilitaka kuomba ila sijui na nini, wamuulize hata yeye mwenyewe.sijawahi kwenda kwake eti kulia shida na namshukuru sana kwa sababu ni mtoto mwenye heshima.

Hivi karibuni kulizuka kwa maneno kuwa mama huyo amekwenda kwa wema na akatakaa kumfungulia mlango ,  mama huyo anasema kuwa wema hajawahi kumvunjia heshima hata siku moja na kila siku alikuwa anatamani kanumba angekuwepo basi angemuomba amuoe wema.

Siku zote nimekuwa nikisema kama Mungu angekuwa amemuweka Steven, yule mimi nilikuwa nimempenda na ningempendekeza awe mkwe wangu.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.