“Marafiki Wabaya Walitaka Kumpoteza Wema”-Mama Wema

Mama mzazi wa staa wa Bongo movie Wema Sepetu, Bi. Mariam Sepetu ‘Mama Wema’ amefunguka na kuwataja marafiki kama watu waliokuwa wanampoteza Wema.

 

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Mama Wema Mama Wema alimuongelea binti yake Wema  ambaye kwa sasa amekuwa kimya huku akionekana kufanya mambo ya maendeleo ikiwemo kufungua duka lake la nguo lililopo maeneo ya Kinondoni jijini Dar.

Wale watu waliomzunguka hawakuwa sahihi, alikuwa na msururu wa watu wakufuata tu mkumbo, wanafuata tu kama mkia vile.

Wema anapendwa, hata hawa unaowaona kila siku wanampinga kwenye mitandao ya kijamii sio kwamba wanampinga, wanampenda sema Wema anakuwa hajui tu“

Lakini pia Mama Wema alifunguka mapenzi aliyonayo kwa binti yake na kumpongeza kwa kufungua duka lake jipya:

Walimpinga hata katika suala hili la duka lakini namshuru Mungu amefanikiwa, amelifungua tayari na leo (juzi) amenialika niende kuona.

Mimi huyu ni mwanangu, nampenda sana na ndio maana hata afanye nini bado nitaendelea kuwa naye bega kwa bega, naamini kabisa sasa hivi ameachana na marafiki wasiofaa na amebadilika”.

Wema amekuwa kimya sana tangu skendo yake ya kusambaza picha zake za faragha kwenye mitandao ya kijamii ambapo kesi yake bado inaendelea kusikilizwa mahakamani.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.