Matonya aeleza sababu ya kuhamia Kenya

Matonya amepinga uvumi kuwa alitoroka Tanzania kwenda Kenya kwasababu anatakikana na polisi kuhusu kesi ya utumizi wa dawa za kulevya.

Hit maker huyo ambaye anajulikana kwa nyimbo kali kama ‘Vaileti’ na ‘Anita’ alidhibitisha kuwa amehamia Kenya akizungumza na vyombo vya habari nchini humu.

Matonya alieleza kuwa yeye hajatoroka mkono mrefu wa serekali kwani yeye hatumii dawa za kulevya na wanaodai hivyo wanamchafulia jina tu.

“Sijatoroka Tanzania kwasababu hiyo, unaona hata listi ambayo imetajwa Matonya hakuwa pale. Matonya ni mtu safi na hizo ni stori zinakuwa kwa ajili ya kuniharibia jina,” Matonya alisema.

Matonya alieleza kuwa alihamia Kenya kwasababu anajihusisha na biashara kadhaa ikiwemo biashara ya kununua na kuuza gari.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.