Mbosso Afungukia Bifu Lake na Aslay

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema chini ya Label ya WCB amefunguka na kuweka wazi kuwa hali sio shwari kati yake na msanii mwenzake Aslay.

Mbosso ameweka wazi kwamba kwa sasa hayupo sawa na muimbaji mwenzake, Aslay ambaye awali alikuwa anafanya naye kazi katika bendi ya Yamoto Band.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Azam, alisema kuwa awali alikuwa anamsupport Aslay katika kazi zake ambazo amekuwa akizitoa lakini yeye amedai alikuwa hasapotiwi na muimbaji huyo.

Baada ya kumsupport Aslay kwa muda mrefu watu wakawa wananimbia mbona wewe unam-support halafu yeye haku-support? umem-follow mwenzako ameku-unfollow. Jifunze kubalance shobo, nikasema kumbe na mimi naonekana namshobokea ngoja na mimi nim-unfollow. Kwa hiyo sasa hivi kila mtu hana urafiki na mwenzake”.

Aslay na Mbosso walikuwa katika Kundi moja la Yamoto Band kwa miaka mingi Lakini walikuja kutengana  kutokana na sababu za kimaslahi ambapo Mbosso alijiunga na Label ya WCB.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.