Mbosso Awalaumu Mashabiki Kwa Video Yake Chafu

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Maromboso au maarufu kama Mbosso ameelekeza lawama kwa mashabiki baada ya video yake kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii.

Siku chache zilizopita video ilisambaa mtandaoni iliyomuonyesha Mbosso akiiwa stejini akitumbuiza kwenye shoo ya Kusi night huku akimbambia msichana mmoja katika staili za kimahaba.

Video hiyo ilisababisha mashabiki kumjia juu Mbosso huku wakiwarushia lawama WCB na kudai wamembadilisha Msanii huyo na kumfundisha tabia mbaya.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5 Mbosso amefunguka hay kuhusu video ile:

Unajua watu wengi wanaamini mimi nimebadilika lakini hakuna kuna baadhi ya vitu vinachangia hasa kwenye shoo inakulazimu ufanye vitu fulani ili watu wafurahi kwaiyo unajikuta unafanya vitu fulani ili shoo ipendeze na watu wafurahi na mashabiki wawe na shangwe na wewe ndio inabidi uwape burudani mashabiki  zako”.

Lakini pia Mbosso amesisitiza kuwa yeye binafsi hakupenda kufanya vile ila kutokana na msukumo wa mashabiki waliokuwa wanampa ukumbini pale akajikuta akifanya vile.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.