Mch. Lusekelo-Nampenda Diamond ni Mnyenyekevu, Simpendi Alikiba ni Jeuri

Mchungaji wa kanisa la Maombezi (GRC) mchungaji maarufu kama Mzee wa Upako ameetaja Diamond kama msanii anayemkubali.

Mch. Lusekelo amefunguka kwenye kipindi cha Maisha Mseto cha Times Fm ambapo ameweka wazi kuwa anampenda Diamond kwa sababu ni mnyenyekevu lakini hampendi Ali Kiba kwa sababu ni mjeuri.

Mimi nampenda sana Diamond kwa sababu ni mnyenyekevu, Simpendi Alikiba kwa sababu ana kiburi, nadhani kwa sababu amekaa Kariakoo”.

Lakini pia Mchungaji huyo hakuishia hapo aliongeza kwa kumsifia Diamond kuwa unyenyekevu wake ndio unamfikisha mbali:

Ukipigia simu Diamond anapokea kwa unyenyekevu ila Alikiba anapokea kwa maringo. Ndio maana Diamond amefika mbali.”

Wasanii hawa wawili wakali wa Bongo fleva wamekuwa wakishindanishwa kwa muda mrefu sana hali iliyosababisha wawili hao kuwa na bifu fulani hivi.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.