Mimi Mars-Napenda Sana Mapenzi

Mwanamuziki wa Bongo fleva na Mshehereshaji (MC) maarufu kama Mimi Mars amefunguka na kuweka wazi kuwa hakuna kitu anapenda duniani kama Mapenzi.

Mimi Mars amefunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv, ambapo amekiri kuwa yeye ni mtu wa mapenzi sana kiasi ya kwamba hata akikutana na jambo lolote linalohusu mapenzi basi huwa Makini.

Mimi napenda sana mapenzi hata kama kuna story ya mapenzi kuna sehemu imeisha ukianza kuwa na Mahusiano na mtu mwingine unaanza upyaa, ina maana uneshasahau yale ya nyuma kimeanza upya Coz you know mapenzi yanarun dunia”.

Mimi Mars anayetokea Kwenye Familia ya Kimuziki kuanzia dada yake Vanessa Mdee anayefanya muziki wa Bongo fleva mpaka dada yake mwingine ambaye pia ni msanii wa nyimbo za injili, ameendelea kufanya vyema na ngoma yake ya ‘Kodo’.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.