Miss Tanzania Afunguka Haya Baada Ya Kurudi Kutoka Miss World

Miss Tanzania mwaka 2018/2019 Queen Elizabeth Makune amefunguka kwa Mara ya kwanza tangu arudi nchini kutokea nchini China kwenye mashindano ya Miss World.

Mashindano ya Miss World yalifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita huko Sanya nchini China ambapo mrembo kutoka Mexico Vanessa Ponce de Leon ndiye aliyetawazwa kuwa Miss World.

Ingawa Miss Tanzania hakufanya vizuri sana na kutoka katika hatua za mwanzoni za mashindano lakini watu wengi walionekana juhudi zake katika kutaka kushinda.

Siku ya Jumatatu Miss Tanzania alirudi nchini na kufanya mahojiano na Millard Ayo, ambapo amesema anawashukuru Watanzania kwa mchango wao, pia amejifunza mengi nchini China na anashukuru kwa matokeo aliyoyapata.

Nimejifunza vitu vingi sana ikiwemo tamaduni, vimenijenga mimi kama mrembo na safari yangu haijaishia hapo huu ni mwanzo tu“.

 

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.