Mkubwa Fela- Wanaopenda Kuona Diamond na Ali Kiba Wana Ugomvi Wameumbuka

Sio jambo la siri kuwa Wasanii wakubwa wa Bongo fleva Diamond Platnumz na Ali Kiba hawaivi chungu kimoja ingawa wenyewe kila mmoja kwa wakati wake amesisitiza  kuwa hana bifu na mwenzake.

Siku ya jana Diamond na Ali Kiba walizua gumzo baada ya kuonekana wakipeana mikono na kusalimiana Kwenye msiba wa marehemu Agnes Masogange.

Meneja wa Diamond na mdau wa muziki wa Bongo fleva Saidi Fella maarufu kama Mkubwa Fela amefunguka na kuweka wazi kufurahishwa na kitrndo cha Diamond kusalimiana na Ali Kiba.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Dizzim Online, Mkubwa Fela alifunguka haya:

Naomba nirudie tena niseme kama ninavyosemaga siku zote watu hawa hawanaga matatizo wala ugomvi kwaiyo hiyo ni baraka kwa nchi yetu na hata muziki wetu wa Bongo fleva kwaiyo cha msingi sisi tuombe dua watu waishi kwa usalama na amani tusipende ile watu wachukiane wapende kugombana sawa ni biashara maana mashabiki wanapenda ushabiki lakini haina maana wasanii hawa wachukiane”.

Lakini pia Mkubwa Fella ameongelea umuhimu wa wasanii hao kuonyeshana ushirikiano kwenye matatizo pale walipokutana Kwenye msiba wa Masogange Lakini pia Mkubwa Fela amewashangaa wachochea bifu na kudai wanaumbuka.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.