Mkuki kwa Nguruwe;-Mama Kanumba
Mama wa marehemu Steven Kanumba anazidi kushika vichwa vya habari katika mitandano kutokana na nafasi anazopata za kuongelea maswala mbalimbali hasa yale yanayohusiana na kifo cha mtoto wake kilichotokea miaka takribani 6 iliyopita.
Mama Kanumba ambae juzi aliwalalamikia wasanii kwa kuwa wamemaliza msiba wa rafiki yao na ndio maana walishindwa hata kutokea katika kumbukumbu ya steven kanumba amefunguka tena na kusema kuwa hata mama yake lulu hakuwahi kukumbuka machungu aliyowahi kuyapata yeye kipindi cha kifo cha kanumba lakini aliumia sana siku ya hukumu ya mtoto wake lulu.
Mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu,mama lulu yeye anaonekana alumia zaidi wakati wa hukumu ya bintiye kabla ya hapo sidhani kama aliguswa na kifo cha mwanangu.-Alisema mama Kanumba lipokuwa akiongea na Globalplublishers