Msanii anayevuma kwa nyimbo chafu Snura Mushi anataka kumrejea Mungu

Ata baada ya kurithi madrasa kutoka kwa babu yake, Snura Mushi aliupea dini kisogo na kuzama kwa mamba ya kidunia.

Msanii huyo amevuma kwa nyimbo zake chafu ambazo yeye hutingisha matako kama mtu aliye pagawa na pepo chafu kutoka kuzimu.

Snura ametamba na wimbo wake ‘Chura’ aliyo toa mwaka jana. Wimbo huo uliwashangaza wengi kutokana na uchafu ulio onyeshwa kwenye video yake.

Ata hivyo Snura sasa anataka kumrejea Mungu, alisema anaamini kwamba mambo ya kidunia yana mwisho wake.

Msanii huyo sasa anataka kuwa mlezi wa madrasa aliyoachiwa na marehemu babu yake iliyopo Yombo Vituka.

“Najitahidi kufanya kazi kwa bidii na maombi yangu kwa Mungu ni aniwezeshe niweze kumtumikia kabla siku yangu ya kufa maana natamani ifike siku niachane na masuala ya kidunia, nijielekeze kwenye dini,” alieleza Snura.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.